Vanessa Ponce De Leon ashinda Miss World 2018

Miss Mexico Vanessa Ponce De Leon amewashinda warembo 118 kutoka nchi mbalimbali duniani na kuvikwa taji la Miss World 2018 rasmi katika shindano lililohitimishwa leo December 8,2018 Sanya nchini China.

Miss Uganda Quiin Abenakyo amefanikiwa kuingia katika Top 5 bora kwenye mashindano hayo akiambatana na mrembo Anastasia Schipanova kutoka Belarus ambaye amekuwa Miss World Europe 2018, mrembo Rosa Montezuma kutoka Panama amekuwa Miss World Americas 2018.
 
Sophida Kanchanarin kutoka Thailand ameshinda taji la Miss World Asia& Oceania na Khadija Robinson kutoka Jamaica amekuwa Miss World Caribbean 2018 huku Miss Uganda akiwa mshindi wa Miss World Afrika 2018, kwa upande wa Miss Tanzania Queen Elizabeth hakuwa na bahati ya kufika nafasi za juu.
 

1 comment:

  1. naona mzee umesha anza na wew kaz yako...twende sasa

    ReplyDelete

Powered by Blogger.