Rais Magufuli atoa agizo kwa Vyombo vya Dola kwa Waliosababisha Akwilina Kupigwa Risasi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli Leo February 18, 2018 ameonesha masikitiko yake kwa Mwanafunzi wa chuo cha NIT Akwilina Maftah ambaye alipigwa Risasi katika maandamano yaliyofanyika February 16 

 Namnukuu President Magufuli “Nimesikitishwa sana na kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwilini wa Chuo cha Usafirishaji (NIT). Natoa pole kwa familia, ndugu, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba huu. Nimeviagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha tukio hili.”

 

No comments

Powered by Blogger.